Uundaji wa maneno ni ujenzi au uzalishaji au utengenezaji wa maneno mapya. Uundaji wa maneno mapya husaidia kuongeza msamiati katika lugha ili kukidhi mahitaji ya mawasiliano. Uundaji wa maneno mapya husababishwa na mabadiliko ya kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni na maendeleo ya kisayansi yanayotokea katika jamii. Kwa mfano tunayo maneno mapya, kama vile ufisadi, uwekezaji, ukeketaji, ujasiriamali na mengine mengi kutokana na mabadiliko ya kijamii.
Kutumia Uambishaji
Kubainisha Mofimu katika Maneno
Bainisha mofimu katika maneno
Uambishaji wa maneno ni kitendo cha kupata maneno kwa kubandika Mofimu kwenye kiini cha neno, uambishaji kutokea kabla ya kiini cha neno au mzizi wa neno. Mfano kiini pig- unaweza kuunda maneno kama inapiga, anayepiga, mpigaji, amepigika nk.
Mofimu zinazobadilika kwenye kiini cha neno huitwa Viambishi.
Katika lugha ya Kiswahili viambishi hutokea kabla na baada ya kiini cha neno.
Mfano
Wanapendana = Wa-na-pendan-a kiini cha neno ni-pend-.
Mofimu zilizobadilisha baada ya kiini –an-na-a viambishi vinavyotokea kabla ya kiini cha neno huitwa viambisha awali au tangulizi. Viambisha vinavyotokea baada ya kiini cha neno huitwa viambishi tamati au fuatishi.
Example 1
Angalia mifano ifuatayo:
Neno | Viambisha Awali | Kiini | Viambisha Tamati |
Unapendelea | u-na- | -penda- | el-e-a |
Waliongozana | wa-li- | -ongoz- | an-a |
Analima | a-na- | -lim- | -a |
anayeiimbisha | a-na-ye | -imb- | -ish-a |
Dhima za Mofimu
Bainisha dhima za mofimu
Baadhi ya dhima za uambishaji ni kama ifuatavyo:
- Kuonyesha upatanisho wa usanifu maana ya maneno yanayozalishwa kutofautiana katika msingi wa kusanifu tu, lakini uhusiano wa maneno hayo hutokana na kiini au mzizi wake uleule.Mfano;Fundisha kiini chake ni fund. Unaweza kuzalisha maneno mengine kwa kutumia mzizi/kiini kilichopo kama vile fundishana, mafundisho, mfundishaji, fundishwa, fundishana.
- Uambishaji huonyesha nafsi
- Uambashaji huonyesha njeo (muda)
- Uambishaji huonyesha urejeshi
- Uambishaji huonyesha ukanushi
- Uambishaji huonyesha hali mbalimbali za kitenzi
Vitenzi vikiambishwa huweza kujenga/kuunda/kuzalisha vitenzi vingine au nomino.
Example 2
Mfano
Vitenzi | Kiini | Nomino | Vitenzi |
Cheza | -chez- | Mchezaji, mchezo | wanacheza/atamchezea |
Piga | -pig- | Mpigaji, Mpiganaji | watanipiga, aliyempiga/wanaompiga |
Uambishaji hutumika kuzalisha viwakilishi na vielezi.
Neno (Kiwakilishi) | Kiini | Kielezi |
Huyu, Huyo | Hu | Humu, humo |
Wangu, wako, wake | wa | |
Hii, hizo, hiki | hi |
Viambishi awali vina dhima ya kudokeza nafsi, njia, idadi urejeshi na ukanushi.Mfano: Hawakulima
- Ha-, kiambishi cha ukanushi
- Ku-, kiambishi njeo/wakati
Viambishi tamati vina dhima mbalimbali hudokeza hali ya utendekaji, ukamilishaji au kimalizio cha neno na kauli za matendo kama vile kutendwa, kutendewa,kutendeka nk.
Dhima:Ukanusho, kutendeana, agizo na mtendwa, ukamilisho, usababishi.
Example 3
Mfano
Neno | Viambishi Tamati |
Anapiga | -a |
Wanapigana | -an |
Asipigwe | -w |
Amempigisha | -ish- |
Viambishi tamati vina dhima ya kutambulishwa mapema/nomino zilizoundwa kutokana na vitenzi.
Neno | Kiini | Viambishi Tamati |
Piga | pig- | -o |
Mchezo | chez- | -o |
Mtembezi | tembe- | -z-i |
Mfiwa | -fi- | -us-a |
By Marco Raphael.
Watanzania ni watumiaji wa lugha ya kiswahili endapo kiswahili kikiondolewa watashindwa kukamilisha mawasiliano je ni madhara gani mengine atapata?
LikeLiked by 1 person
Ndugu Ajuaye shonde
Kwanza salamu kwako najua umesubiri kwa muda mrefu bila kupata jibu juu ya swali lako hapo juu lihusulo madhara yatakayo patikana endapo kiswahili kitaondolewa. Kwanza samahani kwa usumbufu kwa subira yako kwa muda mrefu na hii yote ni kwa sababu ya majukumu mbalimbali ya kijamii
1. Kusaidia kuleta umoja wa taifa zima.
2. Kudumisha utamaduni wa kitanzania kuliko kufuata kasumba.
3. Kufanya Watanzania waamini zaidi mambo yao kuliko kutegemea tu ya kigeni.
4. Kurahisisha upatikanaji wa ajira kwa watumiaji wa lugha hiyo hata nje ya Tanzania .
5. Kukuza sekta ya utalii.
LikeLiked by 1 person
Napenda kazi yako inanifaidi pakubwa mie mwalimu mwanafunzi wa kiswahili kongole sana
LikeLiked by 1 person
Kongole pia kwa kuwa mfatiliaji mzuri wa lugha hii adhimu ya Kiswahili.
LikeLike